Jumapili, 24 Septemba 2017

WOKOVU KATIKA AGANO JIPYA.

SHALOM MPENDWA KATIKA BWANA.

Karibu tena katika blog yako pendwa ya UPENDO WORSHIP "UW"
 Leo tunaenda kujifunza kuhusu wokovu.

Ukisoma Biblia yako katika kitabu cha Efeso 2:8 inasema " nanyi mmeokolewa kwa neema kwa njia ya imani."  yaani tumepata kuokolewa (WOKOVU) kwa NEEMA kwa njia ya IMANI. Hayo ndiyo maneno ya agano jipya yenye kumtukuza Yesu. Ya kwamba ndiye aliyetimiza hayo.

WOKOVU halisi ndio aliouleta Yesus Kristo, yeye ndiye aliyeleta wokovu hapa duniani, na wala hapana mwingine aliyeleta wokovu kama huu. Yesu alikuja kutukomboa kutoka dhambini.

1Petro 2:24 " yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki;na kwakupigwa kwake mliponywa."

Shida kubwa ya watu wengi hawataki kumwamini Yesu, na hata wale ambao wamekwisha mwamini bado wanajiona ni wenye dhambi, na bado wengi wao wanateswa na dhambi, bado shetani anaendelea kuyashikilia maisha yao, leo hii nina habari njema juu yako ya kuwa, ukishaokolewa unasamehewa dhambi na Mungu hatazikumbuka tena hizo dhambi zako. Nawe utapata kuishi kwa ile neema ya Mungu, na hata ikatokea ukaanguka dhambini bado neema ya kukuokoa kutoka dhambini, na hakika utaokolewa na Mungu atakusamehe kabisa.

Waebrania 8:12 " kwasababu nitawasamehe maovu yao, na dhambi zao sitazikumbuka tena"

Leo hii shetani amekamata fikra za wapendwa wengi sana, na kuwakumbusha dhambi zao, na kujiona si kitu machoni pa Bwana, kwakua shetani anawakumbusha dhambi ili wajione ni wenye dhambi, nataka nikwambie kitu, Mungu akishasamehe dhambi zako, azikumbuki tena, na anakupa neema ya kukusamehe na kukuokoa pindi uingiapo kwenye majaribu. Usijione tena mwenye dhambi ndani ya Kristo Yesu, jihesabie mwenye haki, na mwenye neema ile ya kukukomboa kutoka dhambini ili shetani asiishike nafsi yako na kijiona huna kitu machoni pa Bwana maana shetani anakamata fikra za watu ili apate kuwatenganisha mbali na imani ya Yesu Kristo.

Soma Biblia katika kitabu cha Mathayo 11:28 " njooni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. 
Soma Biblia katika kitabu cha Zaburi 68:12 "Na ahimidiwe Bwana, siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu; Mungu ndiye wokovu wetu"

Mpendwa katika Bwana Mungu wetu ndiye mwokovu wetu anayetuokoa na kututua mizigo yetu siku hadi siku, naye anasema twendeni kwake wenye kuelemewa na mizigo naye atatupumzisha, unaweza ukawa unafanya dhambi bila wewe kufahamu, lakini po neema, kadri unavyozidi kumtumainia Mungu, dhambi zinajiachia kila siku, kwamaana hututua mizigo yetu siku kwa siku.

Mungu wetu hajatukomboa tu na dhambi bali alitukomboa na dunia hii mbovu

Wagalatia 1:4 " ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili ya dhambi zetu, ili atuokoe na dunia hii mbovu iliyopo sasa, kama alivyopenda Mungu, Baba yetu"

Hii dunia tunayoishi, ni dunia mbovu yenye kujaa kila aina ya kazi za ibilisi ambaye anafanya kila aina ya njama ili kututenga mbali na Mungu wetu.Ashukuriwe Yesu ametuokoa na kazi mbovu hizi za ibilisi, kwa maana sisi hatukupokea roho ya dunia kwamaana ni mbovu, mija ya kazi za ibilisi ni "kiburi".

Nataka nikwambie kitu mpendwa, kama unasumbuliwa na mizigo ya dhambi, kama unasumbuliwa na kazi mbovu za mwovu ibilisi, wewe uliyejiona si kitu machoni pa bwana kumbuka ipo neema juu yako, ipo neema kwa Yesu Kristo, yeye aliyesema njoeni nyote msumbukao na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzinsha, yeye atuondoleaye mizigo siku hadi siku, hakika ni muweza wa yote kwake aaminiye. Ukimtumainia naye atafanya makubwa katika maisha yako na shetani hatapata nafasi tena.


Mtumishi wa Yesu
@Henry Sebastian Kibanga
Kipaombele > Mathayo 6:33
FB page: UPENDO WORSHIP
INSTAGRAM: UPENDO WORSHIP
http://upendoworship.blogsport.co.id/?m=1


Jumamosi, 16 Septemba 2017

MAMBO YANAYOTOKEA BAADA YA KUOKOKA

SHALOM WAPENDWA KATIKA BWANA

Karibu tena katika blog yako pendwa ya UPENDO WORSHIP

Leo tunaenda kujifunza mambo kadhaa ambayo yanatokea baada ya mtu kuokoka ( kumkubali YESU kuwa BWANA na mwokozi wa maisha yake)

Amini nakwambia kuna mambo mengi sana yanatokea katika ulimwengu wa Roho pindi mtu anapoamua kumpokea YESU KRISTO kuwa BWANA na mwokozi wa maisha yake. Baadhi ya mambo hayo ni;

1: UNAKUA KIUMBE KIPYA

Ukisoma 2Korintho 5:17 "hata imekua mtu akiwa ndani ya Kristo amekua kiumbe kipya, ya kale yamepita, tazama yamekuwa mapya." Yaani unakua umezaliwa mara ya pili, kuzaliwa mara ya pili ni kile kitendo cha mtu kubadilisha maisha yako ya kale kabla ya kumpokea YESU, ila pale tu mtu unapompokea Yesu ndipo unakua umezaliwa mara ya pili.

2: KUINGIA KATIKA UFALME WA MBINGUNI

Yesu akajibu, akamwambia Amin, amin nakuambia, mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa mbinguni. " Yohana 3:3" 
Kwaio tunaona bila ya kuwa kiumbe kipya, bila ya kuzaliwa mara ya pili huwezi kuuona ufalme wa mbinguni. Na ufalme wa mbinguni ndiko kwenye kila kitu na ndiko Mungu anataka tuishi katika ufalme huo wa mbinguni. 
Mathayo 6:33 "Bali utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo yote mtazidishiwa.
Hivyo basi unaona ni jinsi gani ilivyo muhimu mtu kuzaliwa mara ya pili ( kumpokea Yesu Kristo) maana ndipo penye kukupeleka katika Ufalme Wa Mbinguni.

3: UNAKUA MWENYE BARAKA.

Ukisome kisoma kwenye Biblia Waefeso 1:3 inasema " Atukuzwe Mungu, baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo.
Hakika utakuwa mbarikiwa kwa baraka zote za rohoni katika Kristo Yesu.

4: UNAKUA SIO MTUMWA TENA WA MAOVU (DHAMBI), UNAKUA HURU

Ukiwa kiumbe kipya, ukaingia katika ufalme wa mbinguni na kuwa mwenye baraka, Kumbuka Yesu alikufa pale msalabani kwaajili ya dhambi zetu, ile damu iliyomwagika pale msalabani ilitukomboa kutoka kwa yule mwovu shetani, kwa maana huko ndiko kwenye dhambi na kila aina ya uovu, sasa uwezi kuushinda huo uovu kama hujaamua kumkabidhi Yesu maisha yako, hivyo unapoamua kuokoka unakua unaingizwa katika ufalme wake Mungu.
Ukisoma katika Biblia kitabu cha Wakolosai 1:13-14 "Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake, ambayo katika yeye tunaukombozi, yaani masamaha wa dhambi.

Hivyo ukiokoka huru, mwenye kusamehewa dhambi zako zote, na unakua sio mtumwa tena wa dhambi, maana atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi, na mshahara wa dhambi ni mauti.
 " Warumi 6:23"

5: KUONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU

Unapoamua kumpokea Yesu Kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako na kumtumainia yeye, ukimwomba atakupatia Roho mtakatifu ndani yako kwa ajili ya kukuongoza katika maisha yako. Yesu hutubatizwa kwa Roho mtakatifu " Marhayo 3:11 " na ndio ubatizo wenye thamani kubwa sana kwa maana unashuhudia mbinguni na duniani.

Roho Mtakatifu atakuongoza katika
-Maisha yako
-Kukufundisha neno la Mungu
-Hukumbusha neno la Mungu
-Kukufunua akili zako na kuyaelewa maandiko
Kuna mengi sana ambayo Roho mtakatifu atkuongoza ili ukapate kuishi maisha ya kiutakatifu katika ufalme wa mbinguni

Kwakusema hayo, yapo mengi tu amayo hutokea katika ulimwengu wa kiroho pale mtu akiamua kuokoka, mtummoja akiokoka ni shangwe na furaha tupu Mbingun,
Hivyo katika maisha haya hakuna uamuzi mzuri na mkubwa kushunda yote kama mtu anapoamua kumkabidhi Yesu maisha yake, kama kweli unataka kumuona Mungu katika maisha yako. Mkabidhi Yesu maisha yako.


Mtumishi wa Yesu
@Henry Sebastian Kibanga
Kipaombele > Mathayo 6:33
FB: UPENDO WORSHIP
IG: UPENDO WORSHIP
http://upendowotship.blogspot.co.id/?m=1

Jumatatu, 4 Septemba 2017

KUFANYA IBADA KIUTAKATIFU

MAMBO MUHIMU KATIKA KUIFANYA IBADA KIUTAKATIFU

1.MOYO (ROHO)

Moyo unanafasi kubwa sana katika kukamilisha ibada kiutakatifu. Kwamaana moyoni ndiko kutokako mawazo, ndiko kwenye mawasiliano na Mungu, hivyo usipouandaa moyo wako kwa kupokea neno, kusikiliza neno, kuruhusu au kuamini uweza wa Kimungu hakika hutapokea wala kuifanya ibada kiutakatifu. Kwakusema hayo inatupasa kuiandaa mioyo yetu kuwa safi kabisa kwa maana tutamuona Mungu

"Mathayo 5:8" (HERI WENYE MOYO SAFI KWA MAANA WATAMUONA MUNGU)

usipokua na Moyo safi usitegemee kumuona Mungu kwa namna yoyote ile.

Usiwe na moyo (Roho) wa kusita sita, usiingize hofu, wala usiiache imani yako kukaa mbali na moyo (Roho) waako katika kufanya ibada.

Embu fikiria yule mwanamke aliye gusa pindo la Yesu, tazama jinsi alivyouandaa moyo wake kiimani, aliuandaa moyo kiukamilifu kabisa naye alipogusa pindo akapokea uponyaji.
Nasi leo hii tukitaka kupokea miujiza ya Mungu wetu ni lazima kuiandaa mioyo yetu kiukamilifu ili tupate kupokea katika kufanya kwetu ibada.

 2.KUSIFU NA KUABUDU

Hakika Mungu wetu huketi katika sifa, kadri unavyo msifu na kumuabudu ndivyo anavyozidi kujitukuza katika maisha yako. Mnyenyekeeni Mungu, mwabuduni yeye na kulitukuza jinalake. Kwa kusifu na kuabudu katika Roho na kweli ROHO WA MUNGU HUWAALIKA MALAIKA WATAKATIFU KUFANYA KITUO KATI YA MOYO WAKO NA MBINGUNI.

Tazama Paulo na Sila walivyofungwa gerezani, kwajinsi walivyokuwa wakimuamini Mungu (kutoka moyoni mwao) wakaanza kuomba na kumwimbia Mungu nyimbo za kusifu na tazama milango ya gereza ikafunguka. "Matendo ya Mitume 16:25-26"

Tazama jinsi walivyo sifu, Mungu alishuka kati yao kwa maana Mungu wetu huketi katika sifa.
Leo hii watu huona kumsifu Mungu ni kama kitu cha kawaida, kwamfano waimbaji kanisani wanapo sifu, watu huona ni kawaida, watu wanakaa chini (kwenye viti) yaani kanakwamba walilazimishwa kufanya ibada au kwenda kanisani, kwakufanya hivyo usitegemee Mungu ashuke kati yako kama humsifu, hakika kama na wewe ni mmoja wapo hacha kabisa io tabia, inaonyesha ni jinsi gani hata moyoni haupo safi kwamaana laiti ungalitambua toka moyoni uweza wa Mungu wetu mkuu, ungalisimama na kumsifu Mungu ili kuifanya ibada yako kuwa takatifu na kuruhusu Mungu ashuke na kufanya mapenzi yake.

Hakika msifuni Bwana kwa maana fadhili zake ni za milele.

 3.SADAKA

Sadaka ni kitu kimoja cha muhimu sana katika kushiriki ibada kitakatifu, ni ibada iliyo kamilika. Ibada hukamilishwa kwa kumtolea Mungu sadaka, sadaka ni mbegu iliyo bora, hata neno la Mungu lasema nijaribuni kwa matoleo yenu. Matoleo ndio sadaka, unavyomtolea Mungu kile ulicho nacho kwamaana kadri Mungu atakavyo kuongoza hakika unakua unafanya ibada kikamilifu. Tunasema kadri Mungu atakavyo kuongoza tukimaanisha usitoe sadaka kimazoea.  Toa Sadaka kadri Mungu atakavyo kuongoza. Mungu hupendezwa na sadaka umtoleayo.

Embu fikiria Mtu anaishi maisha ya gharama sana lakini akienda kanisani kwavile amezoea kutoa sadaka sh.500 basi kila siku ni hiyo hiyo hakika hutaweza kufanya ibada kamilifu yenye kumpendeza Mungu. Toa sadaka kadri Mungu atakavyo kushuhudia moyoni mwako ili ikapate kumpendeza Mungu wetu.


UPENDO WORSHIP
http://upendoworship.blogspot.co.id/?m=1
servant of Jesus
@Henry Sebastia Kibanga

Jumanne, 29 Agosti 2017

SALA KWA WANAFUNZI

Shalooom Mpendwa katika Bwana.
Karibu tena katika Blog yako pendwa ya UPENDO WORSHIP.

SALA KWA WANAFUNZI.

Ni Asubuhi nyingine yenye kujaa Utukufu, Eh Mungu wangu, wewe ndiye mkuu wa wakuu, mfalme wa wafalme, usiyeshindwa na jambo, uketie patakatifu pa patakatifu.

Nashkuru kwakua umenilinda mpaka kufikia mahali hapa nilipo, kwamaana si kwa akili zangu wala nguvu zangu, ila ni kwauwezo wako, baraka zako na upendo wako kwangu, na kwa kila neema uliyonijalia, vinanipa ushindi kila siku ya maisha yangu.

Tazama. Nakuja mbele zako eh Mungu wangu,

 Neno lako lasema
"usiiache elimu ikaenda zake kwa maana ndio uzima wangu. "(Mithali 4:13)
Nami hakika sitaiacha elimu, tazama nami napendezwa na kuyatenda mapenzi yako, kwakuwa nalitimiza hilo.

Pia neno lako lasema
" utanifanya kua kichwa na wala si mkia, nami nitakua juu tu, sitakua chini" (Kumb. la Torati 28:13)
kwakuyatimiza mapenzi yako kwa kuwa sijaiacha elimu, hayo yote hayanabudi kutokea katika maisha yangu, kwakua nitakua kichwa na wala si mkia katika maisha ya elimu yangu.

kupitia hayo, nami nitaishi maisha ya ushindi ya kielimu.

Eh Mungu wangu nakupenda kuliko kituchochote, nitakutukuza na kukuabudu wewe tu, siku zote za maisha yangu.

@servant of Jesus
@Henry Sebastian Kibanga
http://upendoworship.blogspot.co.id/?m=1

Jumamosi, 26 Agosti 2017

SALA ZITAKAZO KUKOMBOA KATIKA VIFUNGO VYA MWOVU SHETANI

SHALOOM. Mpendwa katika BWANA
Karibu tena katika blog yako pendwa ya UPENDO WORSHIP
Tukapate kujifunza sala mbali mbali za kutukomboa kutoka katika vifungo vya yule mwovu shetani

Ningependa kukumbusha kitu kabla ya kujifunza sala hizi
kumbuka ya kuwa BILA KUWA NA IMANI KATIKA MUNGU, HAKUNA UTAKACHO FANIKISHA.

SALA YA KUIKOMBOA MIGUU KUTOKA KWENYE VIFUNGO VYA SHETANI

“Basi, haya ndiyo asemayo Bwana MUNGU;

Atakuwako adui, kuizunguka nchi pande zote; naye atazishusha chini nguvu zako zikutoke; na majumba yako yatatekwa nyara. Haya ndiyo asemayo BWANA; Kama vile mchungaji apokonyavyo kinywani mwa simba miguu miwili, au kipande cha sikio; ndivyo watakavyopokonywa wana wa Israeli, wakaao Samaria katika pembe ya semadari, na juu ya mito ya hariri ya kitanda” (Amosi 3:11—12).

Maandiko yanatuambia tunapambana na falme na mamlaka na Shetani akitaka kupambana kwa kiwango cha kifalme eneo analolenga ni miguu. Mungu naye akitaka kukuokoa ili uujenge ufalme wake analenga miguu. Kuna mahusiano makubwa kati ya agano la damu ya Yesu na miguu. Hivyo tunatumia damu ya Yesu ili kuikomboa miguu katika ulimwengu wa roho:

Fanya sala hii kwa imani ili Mungu aikomboe miguu yako kutoka kwa adui:
🏽

MWENYEZI MUNGU BABA WA MBINGUNI. ASANTE KWA AJILI DAMU YA YESU ILIYOMWAGIKA KWA AJILI YA UKOMBOZI WANGU. KWA MAMLAKA ULIYONIPA KATIKA DAMU YA YESU KRISTO NINAIKOMBOA MIGUU YANGU KUTOKA KWA ADUI. NINAFUTA MANENO YOTE NA HATI YA MASHITAKA YA SHETANI ALIYOPITISHA KWEMYE MIGUU KWA DAMU YA YESU KRISTO. NINAUYEYUSHA UZITO AMBAO SHETANI AMEUWEKA NATIKA NAFSI YANGU KUPITIA MIGUU KWA DAMU YA YESU KRISTO. NINAONDOA UHALALI WA NGUVU ZOTE ZA GIZA ZOTE ZILIZOPITA KWENYE MIGUU NA NINAFUTA JINA LANGU (AU JINA LA…MTAJE MTU) KUTOKA KATIKA MAAGANO YA URITHI KWA DAMU YA YESU KRISTO. MAGONJWA YOTE YALIYOPITA KATIKA MIGUU SASA NAYAMURU YATOKE KATIKA MWILI WANGU KATIKA JINA LA YESU KRISTO AMEN!!

MSHUKURU MUNGU!


Fanya sala ifuatayo kwa imani ili uikomboe ardhi kwa damu ya Yesu Kristo. Hakikisha unakuwa unatembea kwenye mipaka ya nyumba yako wakati unafanya sala hii:🏽

MWENYEZI MUNGU BABA WA MBINGUNI. ASANTE KWA SABABU UNALITIMIZA NENO LAKO. UMENIAMBIA KUWA MAHALI NITAPOKANYAGA UNANIPA KUMILIKI (Joshua 1:3; Kumbukumbu 11:24—25). NINAMWAGA DAMU YA YESU KRISTO KATIKA ARDHI HII KWA AJILI YA KUONDOA UFALME WA GIZA NA KUWEKA UFALME WA MUNGU (Waebrania 9:22 &Waebrania 10:9) ILI ENEO HILI LITUMIKE KWA AJILI YA KUSUDI LAKO. NGUVU ZOTE ZA GIZA AMBAZO ZINATAWALA ENEO HILI, KWA MAMLAKA NILIYONAYO KATIKA DAMU YA YESU NAZIAMURU ZITOKE. NINAFUTA LAANA ILIYOPO KATIKA ARDHI HII KWA DAMU YA YESU; NINAFUTA KILA UOVU ULIOPATILIZWA  KILA KIZAZI, KIZAZI CHA TATU MPAKA CHA NNE, KWA DAMU YA YESU; NINAFUTA MANENO YOTE YALIYOANDIKWA KWENYE ARDHI ILI NISIFANIKIWE (Yeremiah 22:29—30) KWA DAMU YA YESU KRISTO. NINAFUKUZA KILA WALINZI WA ARDHI KUTOKA KWA ADUI NA NINAAMURU MAPEPO YA ARDHI HII YATOKE KATIKA ARDHI HII KWA DAMU YA YESU. NINATANGUA MAAGANO YALIYOFUNGWA KWENYE HII ARDHI NA NINATENGANISHA KILA MADHABAHU NA VITI VYA ENZI VINAVYOTAWALA KATIKA ARDHI HII KWA DAMU YA YESU KRISTO. NINATOA HUKUMU YA HAKI KWA MIUNGU INAYOTAWALA ARDHI. NINANYUNYIZA DAMU YA YESU NA KUACHAILIA ULINZI WA MBINGUNI KATIKA ARDHI HII KWA JINA LA YESU KRISTO. NAIWEKA WAKFU ARDHI HII ILI MUNGU UUTUMIE KUTIMIZA KUSUDI LAKO KATIKA JINA LA YESU KRISTO AMEN!!

MSHUKURU MUNGU!


Kama umefanya sala hii kwa imani, kama kuna kitu chochote kile Shetani alipitisha kwenye miguu kitaondoka. Kama ulikuwa unapata shida kusoma biblia au kuomba utashangaa wepesi unaoupata.

Ubarikiwe sana Mpendwa Katika BWANA


Jumapili, 20 Agosti 2017

UADUI KATI YA MWANAMKE NA SHETANI.1

SHALOOM Mpendwa katika BWANA.

Karibu tena katika kujifunza neno la Mungu katika blog yako pendwa UpendoWorship


Leo tunaenda kujifunza juu ya uadui uliopo kati ya mwanamke na mwovu shetani.

Labda nianze na kukuuliza swali ambalo nilikua najiuliza hapo kabla, kwanini katika mikutano ya injili, semina mbalimbali za maombezi, na makanisani pia, idadi kubwa sana ya watu wanaosumbuliwa na shetani (mapepo) ni wanawake. Sio kwamba wanaume hawasumbuliwi na mapepo, lakini hapa naangalia idadi kubwa ambayo ni wanawake.
Je! Ulishawahi jiuliza ni kwanini? Bila shaka kwa akili za kibinadamu ni vigumu kutambua hilo, lakini bila shaka, kwa kile chochote kinachoendelea duniani hakika kilishawahi kuandikwa kwenye biblia. Je! maandiko yanasema nini juu ya hili

Ukisoma kwenye kitabu cha biblia Mwanzo 3:13-15 inasema

Mwanzo 3:13 Bwana Mungu akamwambia mwanamke, Nini hili ulilolifanya? Mwanamke akasema, Nyoka alinidanganya, nikala.
Mwanzo 3:14 Bwana Mungu akamwambia nyoka, Kwa sababu umeyafanya hayo, umelaaniwa wewe kuliko wanyama wote, na kuliko hayawani wote walioko mwituni; kwa tumbo utakwenda, na mavumbi utakula siku zote za maisha yako;
Mwanzo 3:15 nami nitaweka uadui kati yako na huyo mwanamke, na kati ya uzao wako na uzao wake; huo utakuponda kichwa, na wewe utamponda kisigino. 

Nyoka anayezungumziwa hapo ni shetani, hivyo basi ukiangalia mstari wa 15 apo ndipo utaona kabisa ya kwamba Mungu aliweka uadui kati ya mwanamke na yule nyoka(shetani). Hivyo basi kwa uzao wa mwanamke atamponda kichwa nyoka, naye nyoka atakuponda kisigino ewe mwanamke. Tufaham ya kuwa uzao wa mwanamke ni wale watoto ambao atakuja kuzaa (mimI na wewe tu uzao wa mwanamke) na uzao wa shetani ni mapepo.

Mpaka kufikia hapo nafkiri ushaanza kupata picha halisi ya kua uadui huu umeanzia wapi, na ni kwanini idadi kubwa wanaoteswa na shetani(mapepo) ni wanawake, hii yote ni kwasabu Mungu alishaweka uadui kati yao. Unaweza ukawa unajiuliza kwanini aliweka uadui. Jibu ni kwamba

Ukisoma Biblia kitabu cha Mwanzo 1:1-6, Hapo ndipo utaona ya kua kwanini Mungu alieka uadui kati ya hawa wawili, kwa maana nyoka alimdanganya mwanamke, akala lile tunda kwa kumwambia hatakufa bali atajua mema na mabaya angali walikatazwa na Mungu wasije kula tunda la mti huo.
Mungu alichukizwa na hiko kitendo kiasi akaweka uadui kati yao.

Baada ya kulifahamu hilo, chimbuko la uadui huo twende moja kwa moja katika biblia kitabu cha Ufunuo 12:1-11 na kuendelea mpaka mstari wa 17 ( Ufunuo 12:1-17)

Ni shauku ya moyo wangu upate kusoma hapo li upate maana halisi ya uadui huo na jinsi ulivyokua ukiendelea.

Ukisoma hapo utapata kuona kuna ishara kuu iliyoonekana kutoka Mbinguni, Mwanamke mwenye mimba akilia kwa utungu na kuumwa katika kuzaa, ikaonekana ishara nyingine na tazama joka kubwa(shetani) na mkia wake wakokota theluthi ya nyota za mbinguni( nyota hizo ni mapepo) na kuziangusha katika nchi, pia na yule joka akasimama kwa yule mwanamke ili azaapo amle yule mtoto wake. Naye yule mwanamke akazaa mtoto mwanamume naye atakayechunga mataifa yote kwa fimbo ya chuma na mtoto wake akanyakuliwa hata kwa Mungu na kiti cha enzi. Je mtoto huyo ni nani? Jibu ni Yesu Kristo. Hapo ndipo likatimia lile andiko lisemalo kwa uzao wako ewe mwanamke utamponda kichwa nyoka(shetani). Yesu alimponda kichwa shetani pale msalabani.

Ukisoma Ufunuo 12:15 utazidi kuona ule uadui jinsi unavyozidi, kwa maana nyoka akazidi kupambana na mwanamke, nyoka akatoa katika kinywa chake nyuma ya huyo mwanamke maji kama mto, ili amfanye kuchukuliwa na mto huo yule mwanamke, mstari wa 16 unatuambia Nchi(ardhi) ikamsaidia mwanamke, Nchi ikaifunika kinywa chake,ikaumeza mto ule alioutoa yule nyoka.

(Nyoka anapambana na mwanamke lakini pia nchi"ardhi" inamsaidia mwanamke na ndomana moja ya vita kuu ya kiroho ipo kwenye ardhi, kwasababu pia ardhi ilimsaidia mwanamke)

mstari wa 17, chuki ikazidi kwa maana yule nyoka(shetani) akamkasirikia yule mwanamke, akaenda zake akafanye vita juu ya wazao wake waliosalia(wazao wake hao ni mimi na wewe) wazishikao amri za Mungu, na kua na ushuhuda wa Yesu.....

Natumaini mpaka kufikia hapo ushapata picha halisi kwanini shetani anapambana sana na mwanamke kwa njia mbalimbali iwe kuharibu mimba,kumpandikizia magonjwa,mapepo,mateso, kumfanya mwanamke kutojitambua na kuishi maisha ya kianasa kama ilivyo hivi sasa,hii yote kwasababu ya ule uadui kwa maana shetani anapiagana na hii vita ili kuwinda kile kilichopo ndani ya mwanamke ili kisije kumponda kichwa. Naye shetani akisha kufanikisha kwa kuharibu kwa mwanamke apo tunasema nyoka amekuponda kisigino.

Yesu alipokuja alipitia kwa mwanamke(kwa uweza wa Roho mtakatifu). Likatimia neno, kwa uzao wa mwanamke shetani atapondwa kichwa.

Ewe mwanamke kumbuka vita hii si juu ya damu na nyama bali ni vita ya kiroho, hivyo tambua Mungu ameweka kitu cha pekee kabisa kupitia kwako, hivyo usiishi kizembe zembe, kila mara kumbuka kuombea uzao wako,ombea familia yako ijayo(kama bado huna mtoto), kila mara ombea ardhi,ombea akili yako isije kamatwa na mwovu,ombea fahamu zako, usihishi kibahati mbaya, wewe ni mtu wa tofauti kabisa,usikubali nyoka(shetani) akuponde kwenye kisigino,ombea watoto wako, usiruhu mateso ya kimapepo(uzao wa shetani) yakutese maishni mwako,ombea kila kitu kinachoitwa kwa jina lako, (naposema ombea kila kitu kinachoitwa kwa jina lako namaanisha hata mchumba uliye naye au maraiki au mumeo kwa maana shetani pia anaweza akawatumia hao hao kuja kukuharibia uzao wako)

 Kumbuka tunaye Yesu muweza wa yote, hakuna ashindwalo, kwake yeye utapata kumponda kichwa shetani kama yeye alivyomponda pale msalabani.

usisahau ku share ili pia na wenzako wapate kushiriki baraka za ibada hii
@Henry Sebastian Kibanga.
Instagram@UPENDO WORSHIP

Alhamisi, 17 Agosti 2017

UPENDO WENYE KUZIPONYA NAFSI ZETU

JIFUNZE KUWA NA UPENDO WA KIMUNGU.

Yawezekana kabisa ukawa unafahamu nini maana ya upendo. Labda kwa kusema hivi,
Upendo ni jinsi vile mtu apendavyo iwe kihisia au kutamania au kuweka kitu au jambo kuwa kipaombele ndio kupenda. Wengine husema upendo ni ile hali ya kuwa na amani moyoni juu ya kitu fulani.
Inawezekana ikawa ivyo lakini ni kwa njia ya kila mtu na kwa jinsi alivyopokea neno upendo.
lakini kuna vyanzo vingi sana vya upendo, nazungumzia vitu ambavyo vinamfanya mtu kupelekea kupenda.

Kuna upendo wa kumpenda mtu kwa sababu ya kitu fulani alicho nacho kwa dhumuni la kusaidiwa au kutimiza haja zako.

Kuna upendo wa kindugu, huu ni ule upendo mtu anampenda nduguye, yupo radhi kwenda kulala nae kitanda kimoja hospitali kwa ajili ya kumuhudumia. ( chanzo ni ndugu, lakini asingekua ndugu yake au rafiki yake asingempenda)

Kuna upendo huwa unaibuka kwasababu tu jinsi mtu anaevyoendesha shughuli zake za kimaisha kutokea kupenda vitu kadha wa kadha. (vyanzo maranyingi huwa ni tamaa,ushawishi nk.)

Ukiangalia kwa makini kuna jinsi nyingi sana watu hupelekea kuwa na upendo juu ya kitu au mtu fulani katika maisha yao. Pia inafikia mahala uo upendo walio nao waweza kupelekea kuharibikiwa kimaisha kwa sababu mbali mbali.
Je ni kwanini upendo huo hupelekea kuharibikiwa au kupata matatizo katika maisha yao. Naweza sema ni kwasababu unakua si upendo ambao Mungu wetu mkuu ametuagiza tuwe nao katika maisha yetu.
Mfano upendo ambao Mungu hajaagiza ni kumpenda mtu kwasababu ya kitu fulani, hii itakupelekea kumtegemea mtu huyo kwa ajili ya shida zako. Na pindi unapomtegemea mtu kumbuka Mungu alisema nini katika kitabu cha Yeremia 17:5.

Je Upendo wa Kweli Ni upi ? Upendo aliotuagiza Mungu tuwe nao ni upi ? Au Mungu wetu ana upendo upi ? ili tuufate upendo wa Mungu wetu.

Ukisoma Yohana 3:16 utapata kuuona upendo ambao Mungu wetu anao.
Upendo wa Agape . Huu ni upendo ambao Mungu ametuagiza (anapenda) tuwe nao, ni ule upendo wa hali ya juu sana, ni upendo ambao Mungu wetu mwenyewe anao,upendo ambao haujivuni, upendo ambao hautampenda mtu tu kwasababu ya kitu fulani, ni upendo wenye kutufanya kuwa watu wa kipekee sana tukiwa nao na tutakua watu watimilifu.

Kunamadhara makubwa sana kama hautakuwa na upendo huu wa kiMungu. Kwa maana kuna baadhi ya watu au watumishi wakishajiona wanuwezo wa kunena kwa lugha, wanombea na kutoa mapepo na unabii, na kusaidia watu wengine na kujiona wapo katika kiwango kizuri sana cha utakatifu lakini bila upendo huu wa kimungu ni sawa na bure. soma 1Wakorintho 13:2. Kwa maana upendo wa kimungu (AGAPE) ni upendo wa kiwango cha juu sana kuliko chochote, upendo usio isha.
tunasema upendo usio isha kawasabu, embu fikiria ukimpenda mtu kwa sababu ya kitu fulani. Je! siku akikosa hiko kitu bila shaka uo upendo utaisha. Lakini upendo wa Mungu wetu hauishi kwamaana anatupenda hadi hivi sasa hata tukimkosea na kumuudhi tukaomba toba yeye hutusamahe kwaajili ya upendo na kwakuwa tunakibali mbele zake.

Embu fikiria jinsi Mungu alivyoupenda ulimwengu hata akamtoa mwanawe wa pekee (YESU), ili kila amwaminie asipotee bali awe na uzima wa milele. Yohana 3:16
Tulikua wenye dhambi lakini kwa ajili ya upendo wa Mungu kutupenda sisi akaamua kumtoa mwanawe wa pekee ili tupate kuokolewa.

Mpendwa katika Bwana napenda nikutie nguvu katika hili, ukapate kua na upendo wa kimungu (AGAPE). Maana bila upendo huu ni sawa na bure.
waweza kujiuliza kwanini bila upendo huu ni sawa na bure ?

Soma biblia katika kitabu cha 1Wakorintho 13:1-3 na kuendelea kadri Mungu atakavyo zidi kukuongoza.
Hapo ndipo utaelewa ya kua bila upendo huu wa kipekee ambao Mungu anataka tuwe nao hakika utaingia katika kumchukiza yeye.
Kwamaana bila upendo huu utakua mtu wa kujisifia,kujiona wewe ndo bora kushinda wengine,kiburi kitainuka juu yako, lakini ukiwa na huu upendo hautakua navyo hivyo vyote kwamaana ukiwa na upendo huu hautajiona kuwa wewe ndio bora kuliko nk. Na ukiwa na upendo huu ambao Mungu hupendezwa nao hakika utaiponya nafsi yako na katika matendo yako yote utakayotenda katika kumuabudu Mungu hakika hayatakuwa sawasawa bure.

Hivyo basi kwa kulitambua hilo ni shauhuku ya moyo wangu ukapate kuwa na upendo wa hali ya juu sana, upendo wa kimungu maana kwa upendo huu utaweza kuishi maisha ya kitakatifu yenye utimilifu. Ikiwa itakuwia vigumu kua na upendo huu. Ningependa nikutie nguvu na uzidi kuomba ( Mathayo 7:7 ) ili ukapate kuishi ndani ya huu upendo wa kimungu na kufunga hila zote za shetani za kukufanya kushindwa kuwa na upendo huu ambao hata shetani mwenyewe hawezi kuuigilizia.

MUNGU NI PENDO NAYE APENDA WATU. TUWE NA UPENDO WAKE ILI TUSIWE SAWA NA BURE.

WOKOVU KATIKA AGANO JIPYA.

SHALOM MPENDWA KATIKA BWANA. Karibu tena katika blog yako pendwa ya UPENDO WORSHIP "UW"  Leo tunaenda kujifunza kuhusu wokovu. ...