Jumapili, 24 Septemba 2017

WOKOVU KATIKA AGANO JIPYA.

SHALOM MPENDWA KATIKA BWANA.

Karibu tena katika blog yako pendwa ya UPENDO WORSHIP "UW"
 Leo tunaenda kujifunza kuhusu wokovu.

Ukisoma Biblia yako katika kitabu cha Efeso 2:8 inasema " nanyi mmeokolewa kwa neema kwa njia ya imani."  yaani tumepata kuokolewa (WOKOVU) kwa NEEMA kwa njia ya IMANI. Hayo ndiyo maneno ya agano jipya yenye kumtukuza Yesu. Ya kwamba ndiye aliyetimiza hayo.

WOKOVU halisi ndio aliouleta Yesus Kristo, yeye ndiye aliyeleta wokovu hapa duniani, na wala hapana mwingine aliyeleta wokovu kama huu. Yesu alikuja kutukomboa kutoka dhambini.

1Petro 2:24 " yeye mwenyewe alizichukua dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki;na kwakupigwa kwake mliponywa."

Shida kubwa ya watu wengi hawataki kumwamini Yesu, na hata wale ambao wamekwisha mwamini bado wanajiona ni wenye dhambi, na bado wengi wao wanateswa na dhambi, bado shetani anaendelea kuyashikilia maisha yao, leo hii nina habari njema juu yako ya kuwa, ukishaokolewa unasamehewa dhambi na Mungu hatazikumbuka tena hizo dhambi zako. Nawe utapata kuishi kwa ile neema ya Mungu, na hata ikatokea ukaanguka dhambini bado neema ya kukuokoa kutoka dhambini, na hakika utaokolewa na Mungu atakusamehe kabisa.

Waebrania 8:12 " kwasababu nitawasamehe maovu yao, na dhambi zao sitazikumbuka tena"

Leo hii shetani amekamata fikra za wapendwa wengi sana, na kuwakumbusha dhambi zao, na kujiona si kitu machoni pa Bwana, kwakua shetani anawakumbusha dhambi ili wajione ni wenye dhambi, nataka nikwambie kitu, Mungu akishasamehe dhambi zako, azikumbuki tena, na anakupa neema ya kukusamehe na kukuokoa pindi uingiapo kwenye majaribu. Usijione tena mwenye dhambi ndani ya Kristo Yesu, jihesabie mwenye haki, na mwenye neema ile ya kukukomboa kutoka dhambini ili shetani asiishike nafsi yako na kijiona huna kitu machoni pa Bwana maana shetani anakamata fikra za watu ili apate kuwatenganisha mbali na imani ya Yesu Kristo.

Soma Biblia katika kitabu cha Mathayo 11:28 " njooni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. 
Soma Biblia katika kitabu cha Zaburi 68:12 "Na ahimidiwe Bwana, siku kwa siku hutuchukulia mzigo wetu; Mungu ndiye wokovu wetu"

Mpendwa katika Bwana Mungu wetu ndiye mwokovu wetu anayetuokoa na kututua mizigo yetu siku hadi siku, naye anasema twendeni kwake wenye kuelemewa na mizigo naye atatupumzisha, unaweza ukawa unafanya dhambi bila wewe kufahamu, lakini po neema, kadri unavyozidi kumtumainia Mungu, dhambi zinajiachia kila siku, kwamaana hututua mizigo yetu siku kwa siku.

Mungu wetu hajatukomboa tu na dhambi bali alitukomboa na dunia hii mbovu

Wagalatia 1:4 " ambaye alijitoa nafsi yake kwa ajili ya dhambi zetu, ili atuokoe na dunia hii mbovu iliyopo sasa, kama alivyopenda Mungu, Baba yetu"

Hii dunia tunayoishi, ni dunia mbovu yenye kujaa kila aina ya kazi za ibilisi ambaye anafanya kila aina ya njama ili kututenga mbali na Mungu wetu.Ashukuriwe Yesu ametuokoa na kazi mbovu hizi za ibilisi, kwa maana sisi hatukupokea roho ya dunia kwamaana ni mbovu, mija ya kazi za ibilisi ni "kiburi".

Nataka nikwambie kitu mpendwa, kama unasumbuliwa na mizigo ya dhambi, kama unasumbuliwa na kazi mbovu za mwovu ibilisi, wewe uliyejiona si kitu machoni pa bwana kumbuka ipo neema juu yako, ipo neema kwa Yesu Kristo, yeye aliyesema njoeni nyote msumbukao na kulemewa na mizigo, nami nitawapumzinsha, yeye atuondoleaye mizigo siku hadi siku, hakika ni muweza wa yote kwake aaminiye. Ukimtumainia naye atafanya makubwa katika maisha yako na shetani hatapata nafasi tena.


Mtumishi wa Yesu
@Henry Sebastian Kibanga
Kipaombele > Mathayo 6:33
FB page: UPENDO WORSHIP
INSTAGRAM: UPENDO WORSHIP
http://upendoworship.blogsport.co.id/?m=1


Jumamosi, 16 Septemba 2017

MAMBO YANAYOTOKEA BAADA YA KUOKOKA

SHALOM WAPENDWA KATIKA BWANA

Karibu tena katika blog yako pendwa ya UPENDO WORSHIP

Leo tunaenda kujifunza mambo kadhaa ambayo yanatokea baada ya mtu kuokoka ( kumkubali YESU kuwa BWANA na mwokozi wa maisha yake)

Amini nakwambia kuna mambo mengi sana yanatokea katika ulimwengu wa Roho pindi mtu anapoamua kumpokea YESU KRISTO kuwa BWANA na mwokozi wa maisha yake. Baadhi ya mambo hayo ni;

1: UNAKUA KIUMBE KIPYA

Ukisoma 2Korintho 5:17 "hata imekua mtu akiwa ndani ya Kristo amekua kiumbe kipya, ya kale yamepita, tazama yamekuwa mapya." Yaani unakua umezaliwa mara ya pili, kuzaliwa mara ya pili ni kile kitendo cha mtu kubadilisha maisha yako ya kale kabla ya kumpokea YESU, ila pale tu mtu unapompokea Yesu ndipo unakua umezaliwa mara ya pili.

2: KUINGIA KATIKA UFALME WA MBINGUNI

Yesu akajibu, akamwambia Amin, amin nakuambia, mtu asipozaliwa mara ya pili, hawezi kuuona ufalme wa mbinguni. " Yohana 3:3" 
Kwaio tunaona bila ya kuwa kiumbe kipya, bila ya kuzaliwa mara ya pili huwezi kuuona ufalme wa mbinguni. Na ufalme wa mbinguni ndiko kwenye kila kitu na ndiko Mungu anataka tuishi katika ufalme huo wa mbinguni. 
Mathayo 6:33 "Bali utafuteni kwanza ufalme wake na haki yake na hayo yote mtazidishiwa.
Hivyo basi unaona ni jinsi gani ilivyo muhimu mtu kuzaliwa mara ya pili ( kumpokea Yesu Kristo) maana ndipo penye kukupeleka katika Ufalme Wa Mbinguni.

3: UNAKUA MWENYE BARAKA.

Ukisome kisoma kwenye Biblia Waefeso 1:3 inasema " Atukuzwe Mungu, baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo.
Hakika utakuwa mbarikiwa kwa baraka zote za rohoni katika Kristo Yesu.

4: UNAKUA SIO MTUMWA TENA WA MAOVU (DHAMBI), UNAKUA HURU

Ukiwa kiumbe kipya, ukaingia katika ufalme wa mbinguni na kuwa mwenye baraka, Kumbuka Yesu alikufa pale msalabani kwaajili ya dhambi zetu, ile damu iliyomwagika pale msalabani ilitukomboa kutoka kwa yule mwovu shetani, kwa maana huko ndiko kwenye dhambi na kila aina ya uovu, sasa uwezi kuushinda huo uovu kama hujaamua kumkabidhi Yesu maisha yako, hivyo unapoamua kuokoka unakua unaingizwa katika ufalme wake Mungu.
Ukisoma katika Biblia kitabu cha Wakolosai 1:13-14 "Naye alituokoa katika nguvu za giza, akatuamisha na kutuingiza katika ufalme wa Mwana wa pendo lake, ambayo katika yeye tunaukombozi, yaani masamaha wa dhambi.

Hivyo ukiokoka huru, mwenye kusamehewa dhambi zako zote, na unakua sio mtumwa tena wa dhambi, maana atendaye dhambi ni mtumwa wa dhambi, na mshahara wa dhambi ni mauti.
 " Warumi 6:23"

5: KUONGOZWA NA ROHO MTAKATIFU

Unapoamua kumpokea Yesu Kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yako na kumtumainia yeye, ukimwomba atakupatia Roho mtakatifu ndani yako kwa ajili ya kukuongoza katika maisha yako. Yesu hutubatizwa kwa Roho mtakatifu " Marhayo 3:11 " na ndio ubatizo wenye thamani kubwa sana kwa maana unashuhudia mbinguni na duniani.

Roho Mtakatifu atakuongoza katika
-Maisha yako
-Kukufundisha neno la Mungu
-Hukumbusha neno la Mungu
-Kukufunua akili zako na kuyaelewa maandiko
Kuna mengi sana ambayo Roho mtakatifu atkuongoza ili ukapate kuishi maisha ya kiutakatifu katika ufalme wa mbinguni

Kwakusema hayo, yapo mengi tu amayo hutokea katika ulimwengu wa kiroho pale mtu akiamua kuokoka, mtummoja akiokoka ni shangwe na furaha tupu Mbingun,
Hivyo katika maisha haya hakuna uamuzi mzuri na mkubwa kushunda yote kama mtu anapoamua kumkabidhi Yesu maisha yake, kama kweli unataka kumuona Mungu katika maisha yako. Mkabidhi Yesu maisha yako.


Mtumishi wa Yesu
@Henry Sebastian Kibanga
Kipaombele > Mathayo 6:33
FB: UPENDO WORSHIP
IG: UPENDO WORSHIP
http://upendowotship.blogspot.co.id/?m=1

Jumatatu, 4 Septemba 2017

KUFANYA IBADA KIUTAKATIFU

MAMBO MUHIMU KATIKA KUIFANYA IBADA KIUTAKATIFU

1.MOYO (ROHO)

Moyo unanafasi kubwa sana katika kukamilisha ibada kiutakatifu. Kwamaana moyoni ndiko kutokako mawazo, ndiko kwenye mawasiliano na Mungu, hivyo usipouandaa moyo wako kwa kupokea neno, kusikiliza neno, kuruhusu au kuamini uweza wa Kimungu hakika hutapokea wala kuifanya ibada kiutakatifu. Kwakusema hayo inatupasa kuiandaa mioyo yetu kuwa safi kabisa kwa maana tutamuona Mungu

"Mathayo 5:8" (HERI WENYE MOYO SAFI KWA MAANA WATAMUONA MUNGU)

usipokua na Moyo safi usitegemee kumuona Mungu kwa namna yoyote ile.

Usiwe na moyo (Roho) wa kusita sita, usiingize hofu, wala usiiache imani yako kukaa mbali na moyo (Roho) waako katika kufanya ibada.

Embu fikiria yule mwanamke aliye gusa pindo la Yesu, tazama jinsi alivyouandaa moyo wake kiimani, aliuandaa moyo kiukamilifu kabisa naye alipogusa pindo akapokea uponyaji.
Nasi leo hii tukitaka kupokea miujiza ya Mungu wetu ni lazima kuiandaa mioyo yetu kiukamilifu ili tupate kupokea katika kufanya kwetu ibada.

 2.KUSIFU NA KUABUDU

Hakika Mungu wetu huketi katika sifa, kadri unavyo msifu na kumuabudu ndivyo anavyozidi kujitukuza katika maisha yako. Mnyenyekeeni Mungu, mwabuduni yeye na kulitukuza jinalake. Kwa kusifu na kuabudu katika Roho na kweli ROHO WA MUNGU HUWAALIKA MALAIKA WATAKATIFU KUFANYA KITUO KATI YA MOYO WAKO NA MBINGUNI.

Tazama Paulo na Sila walivyofungwa gerezani, kwajinsi walivyokuwa wakimuamini Mungu (kutoka moyoni mwao) wakaanza kuomba na kumwimbia Mungu nyimbo za kusifu na tazama milango ya gereza ikafunguka. "Matendo ya Mitume 16:25-26"

Tazama jinsi walivyo sifu, Mungu alishuka kati yao kwa maana Mungu wetu huketi katika sifa.
Leo hii watu huona kumsifu Mungu ni kama kitu cha kawaida, kwamfano waimbaji kanisani wanapo sifu, watu huona ni kawaida, watu wanakaa chini (kwenye viti) yaani kanakwamba walilazimishwa kufanya ibada au kwenda kanisani, kwakufanya hivyo usitegemee Mungu ashuke kati yako kama humsifu, hakika kama na wewe ni mmoja wapo hacha kabisa io tabia, inaonyesha ni jinsi gani hata moyoni haupo safi kwamaana laiti ungalitambua toka moyoni uweza wa Mungu wetu mkuu, ungalisimama na kumsifu Mungu ili kuifanya ibada yako kuwa takatifu na kuruhusu Mungu ashuke na kufanya mapenzi yake.

Hakika msifuni Bwana kwa maana fadhili zake ni za milele.

 3.SADAKA

Sadaka ni kitu kimoja cha muhimu sana katika kushiriki ibada kitakatifu, ni ibada iliyo kamilika. Ibada hukamilishwa kwa kumtolea Mungu sadaka, sadaka ni mbegu iliyo bora, hata neno la Mungu lasema nijaribuni kwa matoleo yenu. Matoleo ndio sadaka, unavyomtolea Mungu kile ulicho nacho kwamaana kadri Mungu atakavyo kuongoza hakika unakua unafanya ibada kikamilifu. Tunasema kadri Mungu atakavyo kuongoza tukimaanisha usitoe sadaka kimazoea.  Toa Sadaka kadri Mungu atakavyo kuongoza. Mungu hupendezwa na sadaka umtoleayo.

Embu fikiria Mtu anaishi maisha ya gharama sana lakini akienda kanisani kwavile amezoea kutoa sadaka sh.500 basi kila siku ni hiyo hiyo hakika hutaweza kufanya ibada kamilifu yenye kumpendeza Mungu. Toa sadaka kadri Mungu atakavyo kushuhudia moyoni mwako ili ikapate kumpendeza Mungu wetu.


UPENDO WORSHIP
http://upendoworship.blogspot.co.id/?m=1
servant of Jesus
@Henry Sebastia Kibanga

WOKOVU KATIKA AGANO JIPYA.

SHALOM MPENDWA KATIKA BWANA. Karibu tena katika blog yako pendwa ya UPENDO WORSHIP "UW"  Leo tunaenda kujifunza kuhusu wokovu. ...