Jumamosi, 26 Agosti 2017

SALA ZITAKAZO KUKOMBOA KATIKA VIFUNGO VYA MWOVU SHETANI

SHALOOM. Mpendwa katika BWANA
Karibu tena katika blog yako pendwa ya UPENDO WORSHIP
Tukapate kujifunza sala mbali mbali za kutukomboa kutoka katika vifungo vya yule mwovu shetani

Ningependa kukumbusha kitu kabla ya kujifunza sala hizi
kumbuka ya kuwa BILA KUWA NA IMANI KATIKA MUNGU, HAKUNA UTAKACHO FANIKISHA.

SALA YA KUIKOMBOA MIGUU KUTOKA KWENYE VIFUNGO VYA SHETANI

“Basi, haya ndiyo asemayo Bwana MUNGU;

Atakuwako adui, kuizunguka nchi pande zote; naye atazishusha chini nguvu zako zikutoke; na majumba yako yatatekwa nyara. Haya ndiyo asemayo BWANA; Kama vile mchungaji apokonyavyo kinywani mwa simba miguu miwili, au kipande cha sikio; ndivyo watakavyopokonywa wana wa Israeli, wakaao Samaria katika pembe ya semadari, na juu ya mito ya hariri ya kitanda” (Amosi 3:11—12).

Maandiko yanatuambia tunapambana na falme na mamlaka na Shetani akitaka kupambana kwa kiwango cha kifalme eneo analolenga ni miguu. Mungu naye akitaka kukuokoa ili uujenge ufalme wake analenga miguu. Kuna mahusiano makubwa kati ya agano la damu ya Yesu na miguu. Hivyo tunatumia damu ya Yesu ili kuikomboa miguu katika ulimwengu wa roho:

Fanya sala hii kwa imani ili Mungu aikomboe miguu yako kutoka kwa adui:
🏽

MWENYEZI MUNGU BABA WA MBINGUNI. ASANTE KWA AJILI DAMU YA YESU ILIYOMWAGIKA KWA AJILI YA UKOMBOZI WANGU. KWA MAMLAKA ULIYONIPA KATIKA DAMU YA YESU KRISTO NINAIKOMBOA MIGUU YANGU KUTOKA KWA ADUI. NINAFUTA MANENO YOTE NA HATI YA MASHITAKA YA SHETANI ALIYOPITISHA KWEMYE MIGUU KWA DAMU YA YESU KRISTO. NINAUYEYUSHA UZITO AMBAO SHETANI AMEUWEKA NATIKA NAFSI YANGU KUPITIA MIGUU KWA DAMU YA YESU KRISTO. NINAONDOA UHALALI WA NGUVU ZOTE ZA GIZA ZOTE ZILIZOPITA KWENYE MIGUU NA NINAFUTA JINA LANGU (AU JINA LA…MTAJE MTU) KUTOKA KATIKA MAAGANO YA URITHI KWA DAMU YA YESU KRISTO. MAGONJWA YOTE YALIYOPITA KATIKA MIGUU SASA NAYAMURU YATOKE KATIKA MWILI WANGU KATIKA JINA LA YESU KRISTO AMEN!!

MSHUKURU MUNGU!


Fanya sala ifuatayo kwa imani ili uikomboe ardhi kwa damu ya Yesu Kristo. Hakikisha unakuwa unatembea kwenye mipaka ya nyumba yako wakati unafanya sala hii:🏽

MWENYEZI MUNGU BABA WA MBINGUNI. ASANTE KWA SABABU UNALITIMIZA NENO LAKO. UMENIAMBIA KUWA MAHALI NITAPOKANYAGA UNANIPA KUMILIKI (Joshua 1:3; Kumbukumbu 11:24—25). NINAMWAGA DAMU YA YESU KRISTO KATIKA ARDHI HII KWA AJILI YA KUONDOA UFALME WA GIZA NA KUWEKA UFALME WA MUNGU (Waebrania 9:22 &Waebrania 10:9) ILI ENEO HILI LITUMIKE KWA AJILI YA KUSUDI LAKO. NGUVU ZOTE ZA GIZA AMBAZO ZINATAWALA ENEO HILI, KWA MAMLAKA NILIYONAYO KATIKA DAMU YA YESU NAZIAMURU ZITOKE. NINAFUTA LAANA ILIYOPO KATIKA ARDHI HII KWA DAMU YA YESU; NINAFUTA KILA UOVU ULIOPATILIZWA  KILA KIZAZI, KIZAZI CHA TATU MPAKA CHA NNE, KWA DAMU YA YESU; NINAFUTA MANENO YOTE YALIYOANDIKWA KWENYE ARDHI ILI NISIFANIKIWE (Yeremiah 22:29—30) KWA DAMU YA YESU KRISTO. NINAFUKUZA KILA WALINZI WA ARDHI KUTOKA KWA ADUI NA NINAAMURU MAPEPO YA ARDHI HII YATOKE KATIKA ARDHI HII KWA DAMU YA YESU. NINATANGUA MAAGANO YALIYOFUNGWA KWENYE HII ARDHI NA NINATENGANISHA KILA MADHABAHU NA VITI VYA ENZI VINAVYOTAWALA KATIKA ARDHI HII KWA DAMU YA YESU KRISTO. NINATOA HUKUMU YA HAKI KWA MIUNGU INAYOTAWALA ARDHI. NINANYUNYIZA DAMU YA YESU NA KUACHAILIA ULINZI WA MBINGUNI KATIKA ARDHI HII KWA JINA LA YESU KRISTO. NAIWEKA WAKFU ARDHI HII ILI MUNGU UUTUMIE KUTIMIZA KUSUDI LAKO KATIKA JINA LA YESU KRISTO AMEN!!

MSHUKURU MUNGU!


Kama umefanya sala hii kwa imani, kama kuna kitu chochote kile Shetani alipitisha kwenye miguu kitaondoka. Kama ulikuwa unapata shida kusoma biblia au kuomba utashangaa wepesi unaoupata.

Ubarikiwe sana Mpendwa Katika BWANA


Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

WOKOVU KATIKA AGANO JIPYA.

SHALOM MPENDWA KATIKA BWANA. Karibu tena katika blog yako pendwa ya UPENDO WORSHIP "UW"  Leo tunaenda kujifunza kuhusu wokovu. ...