Jumanne, 15 Agosti 2017

MAMBO 3 YA KUKUSAIDIA UFANIKIWE KATIKA UFALME WA MUNGU.

LEO TUNAANGALIA JAMBO LA TATU


3. VIPAUMBELE SAHIHI

Kiwango cha mafanikio ya mtu kinategemea vipaumbele alivyo navyo. Kipaumbele cha kwanza tulichopewa na Mungu ni kuutafuta ufalme wake na haki yake na hayo yote tutazidishiwa (Matayo 6:33). Kipimo cha mafanikio ya mtu ni vipaumbele vyake. Maandiko yanasema tukiutafuta ufalme wa Mungu na haki yake uchumi mzuri, afya nzuri, furaha, amani nk tutazidishiwa.

Kwa hiyo kama tunavitafuta hivi vitu, maana yake hatuna vipaumbele sahihi mbele ya Mungu na tunaishi nje ya kusudi lake. Changamoto kubwa katika maisha ni kujua kitu gani cha kufanya. Lakini pia mafanikio yanategemea sana matumizi ya muda. Kama hujafanikiwa katika eneo fulani, tafuta majibu ya maswali yafuatayo:

a. Nini kusudi la Mungu kukuumba? (Mwanzo 1:26).
b. Nini maono ya Mungu juu yako? (Yeremia 1:5).
c. Nini vipaumbele vyako katika maisha yako? (Matayo 6:33).
d. Kwa nini unafanya hicho unachokifanya (nia ya kufanya unachofanya ni ipi)?
e. Je unatumiaje muda wako? (Waefeso 5:16).

Mungu anataka kukusaidia katika maisha yako kwa kutumia mpango wake. Maono ya Mungu juu ya maisha yako yatafanikishwa kwa mpango ambao Mungu ameuandaa. Mungu tayari alikuchagua hata kabla hujazaliwa (Waefeso 1:4—5). Hivyo Mungu alishaweka mpango wake juu ya maisha yako lakini wa kuamua kuishi kwa kiwango Mungu amekupangia siyo Mungu ila ni wewe.

PIA WAPENDWA TUZIDI KUA NA UPENDO KATIKA MAISHA YA UTAKATIFU.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

WOKOVU KATIKA AGANO JIPYA.

SHALOM MPENDWA KATIKA BWANA. Karibu tena katika blog yako pendwa ya UPENDO WORSHIP "UW"  Leo tunaenda kujifunza kuhusu wokovu. ...